Vanessa Mdee kuachia ngoma aliyomshirikisha rapper wa Afrika Kusini K.O wiki ijayo
Akiwa kwenye maandalizi ya show kubwa
atakayoenda kuifanya Nigeria mwezi ujao ‘Gidi Culture Festival’ , staa
wa muziki Vanessa “Vee Money” Mdee ametoa habari nyingine njema kwa
mashabiki wake.
Wiki ijayo Vee Money atapakua moja ya
kazi zilizompeka Afrika Kusini hivi karibuni, safari aliyoenda na Joh
Makini, Jux, Nahreel, Aika pamoja na G-Nako wiki kadhaa zilizopita.
Alhamisi ijayo March 26, 2015 Vee Money
ataachia wimbo na video mpya iitwayo ‘No Body But Me’ aliyomshirikisha
rapper kutoka Afrika Kusini K.O, audio imetengenezwa na Nahreel.
Kwenye Facebook na Instagram ameandika
“Sikuweza kusubiri tena,
Ninafuraha tele ya kuShare wimbo wangu mpya na nyie mashabiki wa Vee.
Wimbo Na Video yangu mpya ambayo nimemshirikisha rapper mkali kinoma
kutoka South Africa K.O mkali wa Cashtime @MrCashtime @MrCashtime
@MrCashtime @MrCashtime – itakuwa maskioni kwako na live kwenye screen
zenu Alhamisi Tarehe 26 March 2015 #NobodyButMe #NobodyButMe
#NobodyButMe produced by my boy @Nahreel.99”
No comments:
Post a Comment