Wednesday 30 September 2015

Roma: Sina taarifa yoyote niliyopokea kutoka BASATA kuhusu kufungiwa ‘Viva Roma Viva’


Kupitia ‘Planet Bongo’ ya East Afrika Radio amesema hana taarifa yoyote aliyopokea kutoka BASATA kuhusu kufungia wimbo wake, Amesema

“Sina jibu la moja kwa moja na napata kigugumizi kwa sababu sina taarifa rasmi kwa kweli, yani finaly mimi nakuwa kama shabiki tu tena, vile shabiki alivyoona ndivyo mimi kama Roma nilivyoona, niliamka tu na mimi nikaona kama kuna chombo kimoja cha habari kimepost katika akaunti ya Instagram, kwamba kuna tamko limetoka BASATA kwamba limefungia nyimbo ya Roma, kwa sababu ambazo walizianisha” - Roma

Aliongeza kuwa pia hafamu utaratibu unaotumiwa na BASATA katika kufikisha taarifa kama hizo kwa wasanii

“Nisiwe muongo sijui taratibu kinakuwa kinatumia kufikisha information zao, kwa sababu kitu ambacho naona ingekuwa rahisi kama artist kabla hajaachia nyimbo yake mpya ama hajafanya kazi yake ya sanaa, iwe inawasilishwa katika hiko chombo, nadhani hapo tungekuwa tunaenda sawa” - Roma

Kwa upande wa pili, Afisa Habari wa BASATA Bwana Aristide Kwizela amesema kuna aina mbili ya kufikisha taarifa hizo

“Kuna kufungia kwa maana ya msanii mwenyewe kuandikiwa, lakini kama kuna taarifa imetoka public kwamba nyimbo za namna hiyo zimezuiliwa, kuna two way either barua kuandikwa kwa msanii au pia kuna public anouncements kwamba wimbo fulani umefungiwa- Kwizela.  

Source: EATV 

Jiunge Nasi na Huku Pia, Kwa Kubofya

 

No comments:

Post a Comment