Tuesday 28 March 2017

Lil Wayne aja na radio ya Young Money, itaanza kuruka leo Jumanne


Baada ya ukimya wa muda mrefu kutoka Young Money, Lil Wayne anakuja na radio ya Young Money.

Kumekuwa na listi kubwa ya wasanii kuwa na radio zao ambazo hutumika kama kuboost kazi zao pindi zinapoachiliwa, wasanii kama Drake, Dj Khaled, Travis Scott, French Ocean na wengine, rapper Lil wayne ameamua kuileta Young Money radio, ila kwa upande wake yeye ajafata nyayo za kuipeleka radio yake kujiunga na Apple Music, Wayne ameingia partner na Dash Radio.

Kupitia kurasa yake ya Twitter Lil wayne aliitangaza rasmi radio hiyo ya Young Money na kusema kwamba itaanza kuruka leo jumanne ya tarehe 28 na kipindi cha kwanza kitakuwa ni Hoody Baby’s new mixtape Kitchen 24.


No comments:

Post a Comment