Wednesday 7 October 2015

Wasanii tunashindwa kunufaika kwasababau hatuna umoja - Nikki wa pili


Akiongea na kipindi cha Planet Bongo cha ‘East Africa radio’ Nikki amesema kutokuwepo kwa umoja wa wasanii mambo mengi yatazorota, hivyo ni lazima kuwe na umoja utakaosimama na kuwatetea wasanii

“Umoja ni kitu cha msingi, kwa sababu bila umoja mambo mengi ya wasanii yatazorota, na kutokuwepo kwa umoja kutatengeneza matundu ambayo wajanja wachache watapitisha mikono yao kwenye hayo matundu na watafaidika nayo, kwa hiyo lazima kuwe na umoja wa wasanii, ambapo utasimama na kuwasemea wasanii”

Pia alitolea mfano wa matokeo waliyopata baada ya wasanii kuungana kipindi cha Katiba, Alisema

“Wasanii wengi pia hawaoni umuhimu wa umoja, kwa hiyo wamekosa msukumo wa kuwa na umoja, na pia chama na chenyewe kimekuwa kimezidiwa sana na kutokuwepo kwa umoja wa wasanii, kwa hiyo kimejikuta nguvu zake zimekuwa chache, lakini umoja ni kitu cha msingi sana, kuna mifano mingi kama wasanii tulivyo ungana tukatoa sauti zetu kwenye katiba tukaona matokeo yake, kwa hiyo mambo mengi ya wasanii yataweza kurekebishwa kukiwa kuna umoja”

Jiunge Nasi na Huku Pia, Kwa Kubofya

  

No comments:

Post a Comment