Friday 2 October 2015

Billnass adai kipindi cha uchaguzi ndio kipindi kuzuri zaidi kwa wasanii kuachia kazi mpya

Msanii wa Bongo Fleva anayefanya vizuri na Track yake ya ‘Ligi ndogo’Billnas amesema kipindi cha uchaguzi ndio kiupindi kizuri zaidi kuachia kazi mpya tofauti na wasanii wengi wanavyofanya kwa madai ya kuwa kipindi hiki cha siasa watazamaji wa runinga na wasikilizaji wa redio wanaongezeka.

BILLLNAS 

Akiongea na kipindi cha XXL cha CloudsFm, Billnas amesema “TUnatofautiana kuamini, mimi naamini kwenye msimu wa siasa ndio usikilizaji wa redio unaongezeka alafu ata uangaliaji wa Televisheni, kuna watu wengi labda walikua wanaangalia televisheni za nje ya nchi lakini ikifika kipindi ichi ndio wanaangalia local channels kwasababu ya mambo ya kisiasa  wajue taratibu nzima za nchi yetu zinavyoenda hususani kipindi hiki cha siasa, unakuta labda wakati mtu anasuburi aangalie taarifa ya habari anaweza akakutana ligi ndogo inapigwa.. kwahiyo naamini usikilizaji umeongezeka..”

Jiunge Nasi na Huku Pia, Kwa Kubofya

 

No comments:

Post a Comment