Wednesday 27 May 2015

Nikk wa Pili kuwania Urais, Hizi ndizo sera zake ambazo angependa Rais awe nazo!

Kampeni aliyo ianzisha msanii kutoka kundi la Weusi ambaye anachukua PHD kwa sasa, Nikk wa Pili ya #Uchguzi kwa Amani ni moja ya kampeni inayo shika kasi kwa sasa baada ya ile ya #Zamu yako 2015 inayo shikiliwa na EATV na EA Radio.

Leo msanii Nikk wa Pili ametoa mtazamo wake endapo kama angekuwa Rais 'Sio kweli kuwa anataka kuwa raisi au kuwania uraisi'. Ameweka sera ambazo zina mashiko kwake.

Soma aliyo yaandika kisha mpe comment yako hapo chini ili akipita aisome

  1. Serikali lazima irudi kuwekeza kwenye uchumi.
  2. Wawekezaji nawapa sector zilizo dumaa hamna uwekezaji wa kuvuna bali wa kuzalisha.
  3. Lectures za vyuo zitarekodiwa na kutakuwa na you tube chanells za accounts, marketi, sociology nakadhalika.......so kwa waliokosa vyuo na mikopo, unaweza ukawa unazitazama....then chuo unakuja kufanya mitihani....vitabu navyo on line.
  4. Shule za vipaji maalumu narudisha, divion one ya kwanza haulipi ada, masomo ya sayansi 60% kwa vitendo.
  5. Mbunge lazima uwe na masters.
  6. Kipimo cha maendeleo ni watu.
  7. Kipimo cha miradi, sera, wizara ni matokeo yake kwa watu.
  8. Ukipatikana na rushwa unafutiwa kazi na vyeti vyako.
credit : tubongetz

    FOLLOW US ON


    No comments:

    Post a Comment