Wednesday, 29 March 2017

Jumatano ya leo: Hizi hapa habari kubwa za magazeti ya michezo Ulaya



Daily Star, linasema mechi kati ya Arsenal ma Man City mwishoni mwa wiki inaweza kuamua hatima ya kocha Arsene Wenger, Inter Milan wanaweza kumtoa Gabriel Barbosa ambaye anatakwa na Liverpool kwa mkopo. Inter Milan wanaangalia jinsi ya kumrudish mlinzi wa Manchester United Matteo Darmian katika ligi ya Serie A, Manchester United na Arsenal wanapigana vikumbo kumsajili nyota wa Villareal Samuel Castillejo, imeripotiwa kwamba Chelsea wanataka kuwapa PSG Diego Costa ili wapewe Javier Pastore.

The Sun, Antonio Conte amemuweka Alexis Sanchez katika orodha ya nyota anaowataka sana kipindi cha usajili. Chelsea wanajipanga kumpa Eden Hazard £300,000 kwa wiki ili kujaribu kumzuia asiende Real Madrid. Manchester United wanajipanga kutuma dau la £40m kujaribu kumsajili Eric Dier wa Tottenham Hotspur. Beki wa zamani wa Mamchester United Paddy McNair amedai kwamba alilazimisha uhamisho wake kwenda Sunderland.

Daily Mirror, Erik Lamela na Mousa Sissoko ni wachezaji ghali katika timu ya Tottenham lakini wote wawili wanahusishwa na kutimkia Italia msimu ujao. Raisi wa Houstom Dynamo amemuonya Wayne Rooney kwamba asitegemee mteremko kama akihamia katika ligi kuu ya nchini Marekani. West Ham wanamuona Rafael Benitez kama mrithi wa Slaven Billic endpo watashindwana naye.

Daily Express, gazeti hili leo limekuja na habari za Manchester United moja inasema Zlatan Ibrahimovich amedokeza kuhusu kubakia United msimu ujao na pia Manchester United wanataka kumsajili kinda wa Ufaransa ambaye pia anatafutwa na Real Madrid Aliou Traoure.

Daily Mail, Manchester United wanamfuatilia kwa karibu kinda wa Celtic Kiernay Tierney ambaye ameanza kuwa gumzo kubwa. Harry Kane anaweza kurejea mapema zaidi ya ilivyotarajiwa katika kikosi cha Tottenham. Ronaldinho Gaucho ameachia wimbo wake wa kwanza na wimbo huo unaitwa Sozinho.

Dailly Telegraph, gazeti hili linasema klabu ya West Ham hadi sasa haina mpango wa kumuongezea mkataba kocha wao Slaven Bilic kutokana na matokeo ya hivi karibuni. Mmiliki wa klabu ya Sunderland amemuambia David Moyes kwamba asiwe na wasiwasi kwani hata timu hiyo ikishuka daraja bado ataendelea kuwa kochwa wao.

The Independent, gazeti hili lina habari isemayo Alexis Sanchez alipokuwa mtoto alikuwa akitembelea jela nchini kwao ili akacheze mpira. Kocha Diego Simeone amesema Antoine Griezman hazuiliwi kuondoka Atletico Madrid.

No comments:

Post a Comment