Tuesday 26 April 2016

Ferooz kuachia ‘Nimejifunza’ unaoelezea mambo aliyopitia alipopata matatizo, awa chini ya Fella


Muimbaji huyo wa zamani wa kundi la Daz Nundaz, atakuwa chini ya usimamizi wa Said Fella. Ferooz amesema wimbo huo unaongelea mambo magumu aliyoyapitia wakati alipokuwa kwenye matatizo na jinsi watu aliowategemea kuwa naye walivyomkimbia.

“Nimejifunza vingi, nilikuwa nipo kimya, nimeexperience mambo mengi, unajua unapokuwa upo kimya, unapokuwa kwenye matatizo, unapokuwa haupo juu yaani unapokuwa haupo kazini unakutana na changamoto nyingi,” ameiambia Bongo5.

“Wazuri wako utawajua na wabaya wako utawajua. Ukisikia wimbo ndio utajua mambo mengi zaidi lakini nimejifunza vitu vingi kutokana na maisha yangu na vitu nilivyopitia hapa katikati.”
Ferooz amesema ameamua kuwa chini ya Mkubwa Fella kwasababu ni mtu ambaye amekuwa akimsupport kwa muda mrefu, hajawahi kumuangusha na ana uelewa mzuri kuhusu tasnia ya muziki.

Kwa upande wake Fella ameiambia Bongo5 kuwa aliwahi kumsimamia Ferooz miaka kadhaa iliyopita kipindi ameachia wimbo ‘Ndege Mtini’ na kumrudisha kwenye chati lakini marafiki ‘feki’ walimshauri ‘ujinga’ na kumpoteza tena.

“Mimi niliona isije Ferooz akala unga tukaanza kusaidia kwenye kula unga. Nimemuita nimekaa naye chini nikamuambia ‘mwanangu sikiliza inabidi sasa twende vile ninavyotaka mimi, cha msingi haya ni maisha yako, ukitegemea marafiki wanakuja wanakuzingua unaenda nao mnaachana ukiwa na maisha magumu unakuja kwangu tena’ basi tukakubaliana na hata nyimbo yenyewe nimeiandika mimi kasema kabisa tunaandika nyimbo inaitwa Nimejifunza. Ukiwa na maisha mazuri huwezi kujua rafiki mbaya, ila ukichoka unajua rafiki mbaya,” amesema Fella.

 -Bongo5

Jiunge Nasi na Huku Pia, Kwa Kubofya


No comments:

Post a Comment