1. Lupita Nyong’o – Kenya
Lupita Nyong’o ni jina maarufu mno duniani kwa sasa. Umaarufu wake kwa
Afrika Mashariki ulianzia kwenye tamthilia ya mwaka 2009, Shuga.
Umaarufu wake duniani, ulitokana na kuigiza filamu iliyoshinda tuzo za
Oscar, ’12 Years A Slave.’
Kwenye filamu hiyo aliigiza kama Patsey, mtumwa wa kike aliyejikuta
akipata shida kubwa kwa kazi ngumu za mashambani. Uhusika wake kwenye
filamu hiyo ulimfanya mwaka jana ashinde kipengele cha muigizaji
msaidizi wa kike bora kwenye tuzo za Oscar. Ushindi huo ulimfanya kuwa
muigizaji wa kwanza kutoka Afrika kuwahi kushinda tuzo hizo za thamani.
Pia aliigiza kama mhudumu wa ndege kwenye filamu ya action ya mwaka
jana, Non-Stop akiwa na Liam Neeson na Julianne Moore. Mwaka huu
ameigiza filamu iitwayo Queen of Katwe na Star Wars Episode VII: The
Force Awakens.
Umaarufu wake ulimpa deals zaidi ikiwa ni pamoja na kuwa kisura wa
kampeni ya Miu Miu akiwa na walimbwende wengine, Elizabeth Olsen, Elle
Fanning na Bella Heathcote. Alionekana kwenye majarida makubwa ya
fashion duniani yakiwemo Dazed & Confused huku akiwa mwanamke wa
pili wa Afrika na wa nane mweusi, kukava jarida la Vogue.
April mwaka jana, jarida la People lilimtaja Lupita kama mwanamke mrembo zaidi duniani katika issue yake ya ’50 Most Beautiful.’
2015, Nyong’o alikava jarida la Lucky, Harper’s Baazar’s (UK) na MujerHoy la Hispania.
Wiki hii Lupita amerejea nchini Kenya ambako alitangazwa pia kuwa balozi
wa taasisi ya WildAid inayojihusisha na kampeni dhidi ya ujangili
hususan wa tembo.
2. Diamond Platnumz – Tanzania
Diamond amekuwa si jina maarufu Afrika Mashariki peke yake na sasa
miongoni mwa wasanii wakubwa kabisa barani Afrika. Mwaka huu peke yake
ametengeneza nyimbo kubwa na collabo na wasanii maarufu Afrika
zilizoshika charts kwenye vituo vya redio na runinga vikubwa. March 27
aliachia video ya wimbo wake wa Mduara, ‘Nasema Nawe’ aliomshirikisha
Khadija Kopa ambao haukuishia kufanya vyema Afrika Mashariki peke yake,
bali Afrika nzima. Hadi sasa video yake imeangaliwa kwenye mtandao wa
Youtube kwa zaidi ya mara milioni 2.7.
Collabo yake kubwa kwa sasa ni ‘Nana’ aliyomshirikisha Flavour ambayo
licha ya kushika chart za redio na TV Afrika ikiwa ni pamoja na kuwa
namba moja kwenye kituo cha Trace TV, video ya wimbo huo ni miongoni mwa
zile zinazoangaliwa kwa kasi zaidi kwenye Youtube barani Afrika, ikiwa
na views zaidi ya milioni 2.1 tangu iwekwe May 29. Bila kusahau mwaka
jana alishirikishwa kwenye nyimbo zilizohit za wasanii wa Nigeria,
likiwemo kundi la Bracket na Waje.
Hivi karibuni tu video mbili za nyimbo alizoshirikishwa na wasanii
wakubwa wa Nigeria zimetoka – Nakupenda aliyoshirikishwa na Iyanya na
Love Boat aliyoshirikishwa KCEE.
Pia aliingia studio kurekodi wimbo aliorekodi na msanii wa Afrika
Kusini, Donald. June 13 alishinda tuzo mbili kwenye KTMA 2015. Mwaka huu
ametajwa kuwania vipengele vitatu kwenye tuzo za MTV MAMA na ni
miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza July 18 kwenye utoaji wa tuzo hizo,
Durban, SA. January mwaka huu staa huyo alikuwa mmoja wa wasanii
waliotumbuiza kwenye tuzo za Glo CAF jijini Lagos, Nigeria.
3. Wema Sepetu – Tanzania
Umaarufu wa Wema Sepetu na kuendelea kutengeneza vichwa vya habari
Afrika Mashariki, unaendelea kuwepo kutokana na uhusiano wake uliokufa
na Diamond miongoni mwa mambo mengine. Wema bado ameendelea kuwa staa wa
kike mwenye mashabiki na ushawishi mkubwa nchini Tanzania.
Mwaka huu alishinda tuzo ya muigizaji wa filamu wa kike anayependwa
zaidi kwenye Tuzo za Watu. Alisafiri hadi nchini Ghana kwenye
kutengeneza filamu na muigizaji wa maarufu wa huko, Van Vicker, ambayo
inatarajiwa kutoka mwishoni mwa mwaka huu. Ameendelea kutengenezwa
vichwa vya habari kutokana na kutangaza nia ya kuwania nafasi ya ubunge
wa viti maalum kupitia CCM, mkoani Singida. Kama mambo yakimwendea
vyema, huenda jina lake mwaka huu likabadilika na kuwa Mheshimiwa Wema
Sepetu.
4. Zari the Bosslady – Uganda
Kabla ya kukutana na Diamond, Zari The Bosslady alikuwa maarufu nchini
Uganda. Alijulikana kwa urembo wake na utajiri mkubwa aliokuwa nao
kupitia aliyekuwa mumewe, Ivan. Alifahamika kama mwanamke anayemiliki
magari ya kifahari, mijengo na biashara kubwa. Umaarufu wake umekuja
kukua zaidi baada ya kukutana na Diamond Platnumz na kuanzisha uhusiano
ambao sasa umewafanya kuwa couple yenye nguvu zaidi Afrika Mashariki.
Kwa sasa wawili hao wanatarajia kupata mtoto wao wa kwanza. Mtoto huyo
bila shaka ana nafasi kubwa ya kuwa mtoto maarufu zaidi Afrika
Mashariki.
5. Vanessa Mdee – Tanzania
Vanessa anafahamika kama msanii wa kike kutoka Afrika Mashariki
anayejituma zaidi kuliko wote. Mwaka huu ameshiriki kwenye kampeni
nyingi za kimataifa. Alishiriki kwenye kampeni ya One Organisation
ambapo aliungana na wasanii wengine wa Afrika kuimba wimbo uitwao Strong
Girl. Pia aliungana na mastaa wakiwemo Lupita Nyong’o, Hasheem Thabeet,
Jacqueline Ntuyabaliwe na Alikiba kama mabalozi wa WildAid na kampeni
dhidi ya mauaji ya tembo.
Mwaka huu ametajwa kuwania kipengele cha msanii bora wa kike kwenye tuzo
za MTV MAMA. Wimbo wake ‘Nobody But Me’ aliomshirikisha rapper wa
Afrika Kusini, K.O, ni miongoni mwa nyimbo zinazofanya vizuri Afrika kwa
sasa. Mwezi ujao ataonekana kwenye jarida maarufu la Marekani la
Essence kwenye toleo lake la dunia (global issue). Ni balozi wa Samsung
na Crown Paints.
6. Millen Magese – Tanzania
Happiness Millen Magese @ladivamillen amejipatia umaarufu mkubwa mwaka
huu kutokana na kuwa balozi kwenye kampeni aliyoanzisha mwenyewe ya
tatizo la Endometriosis ambalo limepelelekea afanyiwe upasuaji kwa
takriban mara 13 na kumfanya awe mgumba. Millen ameanzisha kampeni ya
kukuza uelewa wa ugonjwa huo na kuwataka wanawake wenye tatizo hilo
kutooana aibu kujitokeza kuomba msaada lakini pia kuwataka wanaume wenye
watu wao wa karibu walio na tatizo hilo kuwavumilia. Kutokana na
jitihada hizo pamoja na kuwa mstari wa mbele katika kusaidia watu
wasiojiweza, June mwaka huu alitunukiwa tuzo ya Global Good ya BET
Awards.
7. Eddy Kenzo – Uganda
Jina la Edrisa Musuuza maarufu kama Eddy Kenzo halikuwa maarufu sana kwa
Tanzania na Kenya kabla ya June mwaka huu kushinda tuzo ya BET ((Best
Viewers’ Choice International Act). Anahamika zaidi kwa hit yake Sitya
Loss. Wimbo huu ulifahamika duniani kupitia video ya Youtube ya vijana
wa mtaani waliokuwa wakicheza wimbo huu. Video hii ilikuwa maarufu kiasi
cha kuwepo na ombi (petition) ili vijana hao waweze kuhojiwa kwenye The
Ellen DeGeneres Show. Hadi sasa video hiyo ina views zaidi ya milioni
11. 9.
Kenzo ameshatumbuiza kwenye majiji 15 ya Marekani. Ametembelea na
kutumbuiza kwenye majiji kibao duniani. Alitumbuiza kwenye fainali za
mataifa ya Afrika.
8. Sauti Sol – Kenya
Bien-Aimé Baraza, Willis Chimano, Delvin Mudigi na mpiga gitaa wao Polycarp Otieno ndio wanaunda kundi la Sauti Sol.
Mwaka huu walitajwa kuwania tuzo za BET japo hawakufanikiwa kushinda.
June 13, walichukua tuzo ya wimbo bora wa Afrika Mashariki kwenye KTMA
2015 na wimbo wao uliokuwa anthem ya Afrika Mashariki, ‘Sura Yako.’
Mwaka huu wanawania kipengele cha kundi bora kwenye tuzo za MTV MAMA.
Kwa sasa wapo kwenye ziara ndefu nchini Marekani.
9. Alikiba – Tanzania
King Kiba kama anavyojiita, aliufungua mwaka 2015 kwa kishindo na hakuna
anayeweza kubisha kuwa jamaa huyu ana ushawishi mkubwa nchini Tanzania.
Milango yake ya umaarufu nje ya Tanzania imefunguka tena mwaka huu
baada ya kuwa kimya kwa takriban miaka mitatu.
Video ya wimbo wake ‘Chekecha Cheketua’ ilichezwa kwa mara ya kwanza
kwenye kituo cha Trace Urban na kuendelea kupata rotation ya mara tano
kwa siku. Mwaka huu Alikiba alishinda tuzo ya muimbaji wa kiume
anayependwa kwenye Tuzo za Watu na kushinda tuzo takriban sita kwenye
KTMA 2015.
Mwaka huu pia ameungana na wasanii wengine wa Afrika kwenye msimu wa
tatu wa kipindi cha Coke Studio Afrika huku akitengeneza timu na msanii
wa Kenya, Victoria Kimani. Pia aliungana na Lupita Nyong’o, Vanessa Mdee
na K-Lynn kama balozi wa WildAid katika kampeni dhidi ya mauaji ya
tembo.
10. Idris Sultan – Tanzania
Ushindi wa $300,000 wa shindano la Big Brother Africa mwaka jana,
umemfanya Idris kuwa miongoni mwa mastaa wakubwa Afrika kwa sasa.
Japokuwa hajaanza kufanya miradi mingi, ukubwa wa shindano hilo
umeendelea kuliweka jina lake kwenye headlines. Lakini pia uhusiano wake
na mshiriki mwenzie wa shindano hilo, Samantha umewafanya wawili hao
kuokota headlines za hapa na pale kwenye vyombo vya habari vya Afrika.
Idris anafahamika kwa vituko vyake na huenda akawa na nafasi kubwa ya
kuingiza fedha nyingi kupitia kipaji hicho miongoni mwa vingi alivyo
navyo.
-Bongo 5
No comments:
Post a Comment