Tuesday 26 May 2015

Fareed Kubanda 'Fid Q' asema kwa hapa Bongo hakuna wa kushindanishwa naye!


Fid Q na Joh Makini ni marapper ambao wamekuwa wakichukuliwa kama hawaivi chungu kimoja, na wakati mwingine wamekuwa wakishindanishwa na mashabiki wanaotaka kujua nani mkali zaidi ya mwenzake.
Fareed “Fid Q” Kubanda ametoa mtazamo wake wa kile anachodhani kuwa sababu ya mashabiki wa muziki wa Hip Hop kumshindanisha na rapper mwenzake Joh Makini kwenye mitandao.


“Labda ni kwasababu (Joh) anaweza akawa ni msanii ambaye anafanya vizuri kwahiyo wanakuwa wanamshindanisha na msanii mwenzake mwingine (Fid) ambaye anafanya vizuri, lakini sidhani kama kuna kitu personal na siko katika position kuamini mi nahitaji kushindanishwa na Joh.” Alisema Fid kupitia 255 ya XXL ya Clouds Fm.

Fid amesema kuwa yeye ni msanii ambaye hawezi kushindanishwa na msanii mwingine yeyote kutokana na kile anachokifanya kuwa tofauti na wanachofanya wasanii wengine wote, na pale anaposhindanishwa huwa anaona kama amedharaulika.

“Nadhani wanaoshindanisha wajifunze kuwa wanafatilia watu wanaotaka kuwashindanisha kwanza, mi nadhani niko tofauti kidogo na wanamuziki wengi sana ambao wanafanya Hip Hop na hiyo haijalishi kama ngoma zangu zinapigwa sana redioni au hazipigwi. 
Kibongobongo kiukweli mi sidhani naweza kushindanishwa na mtu na wala siwezi kujisikia vizuri, na mara nyingi naposhindanishwa na mtu naona kama nimedharaulika hivi, sio kwasabbu huyo mtu mwingine ni dhaifu No!, kwasababu mi nafanya kitu cha tofauti sana…nazingatia zaidi uandishi, nafanya show mpaka kesho na ngoma kama dotcom, dotcom ni ngoma ambayo nimeitoa 2003, 2004. 

Katika show zangu hizo hizo napigaga Mwanza Mwanza ambayo imetoka 2005 ilikuwa nyimbo bora ya Hip Hop…saizi ni 2015 tunaongelea miaka tisa iliyopita na zaidi, basi hebu tuangalie basi na hao wengine ambao wanataka kunishindanisha nao wana vibao vyao vina miaka hiyo tisa ambavyo wanaweza kufanya sasa hivi vingapi?”

Kuhusu kama amewahi kuwa na matatizo yoyote na Joh Makini:
“Sijawahi kuwa na matatizo na Joh Makini, nadhani matatizo yanayosikika kwa watu unajua fans wana vitu vyao, ukiingia sehemu mara utakutana na mtu kaweka picha sijui Fid Q vs Joh Makini nani noma, nadhani vitu kama hivyo ndo waga vinatengeneza chokochoko nyingi nyingi ambavyo mtu kama sio mtu wa kufikiria vyema unaweza kuchukulia personal.”

No comments:

Post a Comment