Friday, 7 November 2014

Chid Benz na Fid Q kufanya album ya pamoja, Chid aizungumzia project hiyo

Takribani miezi mitatu imepita tangu Chidi Benz azungumzie kuhusu harakati zake za kufanya album na mkali wa hip hop Fid Q, Fareed vs Rasheed. Leo hii Ndani ya XXL ameongelea alipofikia juu ya kukamilisha album hiyo

Album hiyo ambayo imetokana na idea ya Chidi Benz tayari imeshaanza kufanyiwa kazi ambapo ngoma moja imeshakamilika lakini Chidi pia ameongelea kuhusu yeye mwenyewe na ratiba ya kuingia studio.

"kwasababu tulisha record ngoma moja so nafkiri sasa, now tunatakiwa tuingia mzigoni so nahisi the project itakuwa noma and me najitayarisha kuingia ingia vistudio napitia vistudio viwili vitatu hapa na pale nini, kwahiyo natafuta bado, nahisi nikijakupata msumari ntakuja tu kusema jamani eeh baada ya huu ni huu sasa hivi niko nautengeneza tengeneza na create," amesema Chidi

Ya tunafanya album mzima inabidi tupge mikono tu, chidi na fid kwasababu ni  Rasheed na Fareed  kwahiyo tumeamua tu sisi wenyewe kufanya kitu..........
Ni idea yangu nilikuwanayo kabla sijatoa ngoma wala sikujua kama nitakuwa busy na ngoma kwahiyo nilikuwa najua kwamba kwa kipindi ambacho nitakuwa nimekaa nirecord project na Fid so ya imekuja imekuwa ratiba imebaki pale pale tunafanya, tuna mpango tu wa kupiga ngoma za ajabu sana." alimalizia  Chidi

JOIN US 

FACEBOOK/ OMARYRAMSEY

TWITTER/ @RAMSEYOMARY



No comments:

Post a Comment