Wednesday 20 March 2019

Mapya yaibuka ndoa ya Bieber na mrembo Hailey

Ndoa ya staa wa muziki wa RnB na Pop, Justin Bieber na mpenzi wake Hailey Baldwin iliyokuwa ifungwe ndani ya mwezi ujao imesogezwa mbele hadi pale watakapo tangaza tena.

Kwa mujibu wa TMZ, umeripoti kuwa wapenzi hao wamelazimika kuipeleka mbele ndoa yao kwasababu za kiafya zinazomkabili nyota huyo. TMZ ilielezwa na chanzo cha karibu cha nyota huyo.

Iliripotiwa kuwa, Juma lililopita msanii huyo alipost picha yenye ujumbe wa kuwataka mashabiki wake wamuweke kwenye maombi kwani anapitia changamoto ya kiafya japo hakutaka kuweka wazi ni ugonjwa gani.

Hadi sasa hii imekuwa mara ya nne wapendanao hao wamekuwa wakihairisha ndoa yao kwasababu mbalimbali zisizowekwa wazi.

“Watakuwa na harusi hatimaye, lakini hii sio lengo lao sasa,” kwa mujibu wa chanzo kilichoiambia TMZ. “Wao watasubiri mpaka Justin atakapojisikia vizuri na anafurahi juu ya kupanga ndoa yao tena.

Mwezi uliopita, ni wazi kwamba Justin alikuwa anapokea matibabu kwa ajili ya unyogovu kwa sababu amekuwa amejeruhiwa na umaarufu hivi karibuni. ukweli ni kwamba mashabiki hutengeneza kila hoja, nk. Yeye bado anapokea matibabu, ndiyo sababu harusi sio kipaumbele cha juu kwa wanandoa. Justin bado anapokea matibabu kwenye pwani zote mbili lakini muda sio mrefu atakuwa sawa,” chanzo hicho kinasema.

“Yeye sana, anazingatia kupata nafuu. Anataka kuwa mahali pazuri kwa ajili yake na Hailey. Yeye bado ana imani kwamba atafunga ndoa.“

No comments:

Post a Comment